Pages

Showing posts with label KITAIFA. Show all posts
Showing posts with label KITAIFA. Show all posts

August 19, 2014

TASWIRA PICHA KUTOKA VIJIJINI! MWAKA 2014

Picha ni Moja ya Mikoa Maarufu Nchini Tanzania

Mama Akiwa Jikoni na Mwanae,Anaendelea na Upishi. je haya ndio maisha bora kwa kila mtanzania ?

JIULIZE KISHA UJIJIBU.
TUNAO WAWEKA MADARAKANI WAO HUISHI MIJI MIKUBWA KAMA DAR, ARUSHA ,MWANZA

KIKWETE AMPONGEZA BINTI NEEMA




June 21, 2014

MAJINA YA WANAFUNZI WALIO CHAGULIWA KWENDA KIDATO CHA TANO 2014

June 08, 2014

TOLEO MAALUMU KWA MKOA WA MBEYA

Mbeya is a city located in southwest Tanzania, Africa. Mbeya's urban population was 280,000 in 2005. Mbeya is the capital of the surrounding rural Mbeya region (population, with Mbeya, totals approx. 2 million).
Mbeya is the first large urban settlement encountered when travelling overland from the neighbouring nation of Zambia. Mbeya is situated at an altitude of 1,700 meters (5,500 ft), and sprawls through a narrow highland valley surrounded by a bowl of high mountains. The main language is colloquial Swahili, and the English language is extensively taught in schoolsFollowing the 1905 gold rush, Mbeya was founded as a gold mining town in the 1920s. The TAZARA railway later attracting farming migrants and small entrepreneurs to the area. Mbeya and its district was administered by the British until 1961. Mbeya Region was created in 1961. Mbeya City is now a growing metropolis and business centre for the southern regions and the neighbouring countries of Malawi, Zambia and Congo. The City is well connected with an all-weather road that forms part of the "Great North Road" running from Cape Town to Alexandria. The City has several tribes including the Safwa, Nyakyusa and Nyiha, all being agricultural peoples. Mbeya also boasts as one of the regions that form the bread basket of Tanzania.
Local government is administered via the Mbeya Urban District authority and a Regional Commissioner.
Mbeya has weather with enough rainfall and fertile soil which enable it to be thelargest producer of maize, rice, bananas, beans, potatoes (Irish & sweet), soya nuts and wheat in the entire country. Tanzania has a free market in agricultural produce, and Mbeya transports vast amounts of its maize to other areas of Tanzania. There is also extensive animal husbandry, with dairy cattle predominating. Mbeya is also the biggest producer of high-value export and cash crops in Tanzania; those crops are coffee (arabica), tea, cocoa, pyrethirum and spices. There is some smallholder cultivation of tobacco. Firewood is collected by women and girls, from the wooded valleys and mountainsides. Bamboo is naturally abundant in the forests, and there are plans to teach local people about this versatile plant and its many uses. Some gold is still mined in the rural Chunya District, by artisan miners.
Mbeya is considered to be heading the Southern Highlands Regions, that's why there is a Mbeya Referral Hospital which serves the whole of the Southern Highlands regions, Bank of Tanzania BOT, Mbeya Cement Company, Afri Bottlers Company Coca-Cola Company, SBC Tanzania Ltd Pepsi Cola Company, Tanzania Breweries Limited, NMB, TIB, Mbozi Coffee Curing Limited, Tukuyu Tea Company, Tanzania Oxygen Limited TOL - KYEJO, CRDB all these serve as zonal representative for southern Highlands. There are also a number of companies and statutory organisations with zonal offices in Mbeya.

Besides a growing number of secondary schools, Mbeya has some institutes of higher learning education. Among the better known ones are
  • Teofilo Kisanji University is a young institution of the Moravian Church in Tanzania offering courses in theology,business, arts, sciences and educational studies, as well as training pastors and. Since 2005, it has grown out of the earlier Moravian Theological College. The college is situated at Soweto suburb.
  • Mbeya University of Science and Technology (MUST) formerly known as Mbeya institute of Science and Technology (MIST) is a public institution offering degrees, advanced diplomas, and ordinary diplomas in various engineering disciplines. The College is at Iyunga area.
  • Mzumbe University (MU) Mbeya Campus is situated in Forest area next to the Bank of Tanzania. This public University offers bachelor degrees and diplomas in law and business, as well as providing evening programs in postgraduate studies.
  •  

March 11, 2014

MADEREVA WATWANGANA KWA KUTOELEWANA BARABARANI


Madereva Juma na John wakichapana makonde hadharani.
…Akiokota jiwe kumshushia kipigo John aliyedaiwa kutaka kusababisha ajali.
Juma (kulia) akirusha matusi kwa John.
Dereva Juma akimshusha John kutoka kwenye gari lake.
 Watu wakijaribu kumzuia Juma asimshushie kipondo John.
Vidume hao wakiangaliana baada ya kuzipiga.
Gari  la Kulwa.
Daladala lililokuwa likiendeshwa na Hamis.
DEREVA wa daladala Juma Hamis na John Kulwa aliyekuwa na Toyota Canter wamenaswa na kamera yetu wakichapana makonde hadharani pande za Mwenge jijini Dar, kwa kutoelewana.  Hamis alikuwa akiendesha daladala linalofanya safari zake kati ya Kunduchi na Mwenge lenye namba za usajili T 968 AGP ambapo Kulwa alikuwa na gari aina ya Toyota Canetr namba za usajili T945 AM.

CCM YAPULIZA KIPYENGA CHALINZE

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Chalinze kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ridhwan Kikwete akijaza fomu ya kugombea jimbo hilo.

MWANACHUO AUAWA KWA RISASI

Jeneza lenye mwili wa Dorryce Lwena.
MAJONZI, huzuni na masikitiko vimeikumba familia ya Lwena kufuatia mtoto wao mpendwa Dorryce Lwena (27) kufariki dunia kwa kupigwa risasi mkono wa kushoto na ubavu wa kushoto na watu wasiojulikana, Uwazi lilifuatilia.

Tukio hilo la kusikitisha lilitokea mwanzoni mwa mwezi huu, saa tatu usiku, Uwanja wa Edosi, Kitunda, Ilala hatua chache kutoka nyumbani kwa marehemu huyo.
Siku ya tukio, Dorryce ambaye ni mwanafunzi wa Chuo cha…
Stori: Makongoro Oging’ na Harun Sanchawa
MAJONZI, huzuni na masikitiko vimeikumba familia ya Lwena kufuatia mtoto wao mpendwa Dorryce Lwena (27) kufariki dunia kwa kupigwa risasi mkono wa kushoto na ubavu wa kushoto na watu wasiojulikana, Uwazi lilifuatilia.
Jeneza lenye mwili wa Dorryce Lwena.
Tukio hilo la kusikitisha lilitokea mwanzoni mwa mwezi huu, saa tatu usiku, Uwanja wa Edosi, Kitunda, Ilala hatua chache kutoka nyumbani kwa marehemu huyo.
Siku ya tukio, Dorryce ambaye ni mwanafunzi wa Chuo cha Uhasibu Singida (DSA), alikuwa akitoka Kariakoo kununua vifaa vya kwenda navyo chuo siku mbili mbele lakini kifo kilimkuta akiwa anakaribia kufika nyumbani.
Mama mzazi wa Dorryce akiwa na simanzi wakati wa mazishi ya mwanaye.
Kama ilivyo ada, baada ya kujulishwa tukio hilo la kikatili, waandishi wa Uwazi walifika eneo la tukio na kufanya mahojiano na baba wa kufikia wa marehemu ambaye alikuwa akiishi naye baada ya baba mzazi kutengana na mama yake.
Baba huyo aliyejitambulisha kwa jina moja la Maganga alikuwa na haya ya kusema:
“Ilikuwa Jumamosi, Machi Mosi, mwaka huu, saa tatu usiku nikiwa karibu na kwangu, mke wangu (mama wa marehemu) alinipigia simu akaniambia kuna risasi zimepigwa karibu na nyumba yetu, nikamwambia haraka sana wafunge milango na mtu asitoke nje hadi itakapojulikana kuwa risasi hizo zilikuwa za nini.
Ndugu na jamaa wa marehemu wakilia kwa uchungu wakati wa mazishi.
“Muda mfupi baada ya kuongea na mke wangu, dada wa Dorryce alinipigia simu akiniambia nirudi nyumbani haraka kwani Dorryce amepigwa risasi na amefariki dunia.
“Nina gari, niliingia ndani yake haraka tayari kwa safari ya kurejea nyumbani. Nikiwa nakaribia nyumbani niliona kundi la watu, nilisogelea eneo hilo na kukuta mwili wa Dorryce umelala katika dimbwi la damu.
“Nilikuta familia yangu, akiwemo mama wa marehemu wakilia kwa uchungu. Iinibidi nikatoe taarifa Kituo Kidogo cha Polisi Kitunda, nao walinishauri niende Kituo cha Polisi Stakishari.

“Polisi walifika eneo la tukio na kufanya michoro kisha wakauchukua mwili hadi Hospitali ya Taifa Muhimbili.
“Mke wangu ana hali mbaya sana jamani. Tangu tukio hilo amekuwa akizimia mara kwa mara, presha inapanda na kushuka. Naombeni msimhoji,” alisema kwa masikitiko makubwa baba huyo.
Alisema mpaka siku hiyo familia ilikuwa haijui chanzo cha mauaji hayo.
Akasema: “Ninachokumbuka mimi siku hiyo mke wangu alimkataza marehemu asiende Kariakoo lakini alikataa, akasema kwa vile Jumapili atakwenda kanisani na Jumatatu ndiyo safari ya kurudi chuo, afadhali aende siku hiyo.”
“Ila wakati marehemu yupo chuoni alizaa na mwanaume mmoja ambaye tulimtaka amhudumie mtoto kwa vile mama yake bado anasoma lakini alikataa, hivyo marehemu aliamua kumchukua mtoto na kumpa. Hadi hapo tukawa hatuna uhusiano naye mzuri,” alisema mzee huyo.
Waandishi wetu walifanya mahojiano na majirani kutaka kusikia kama wanajua lolote juu ya tukio hilo ambapo baadhi yao walisema mauaji hayo hayajawahi kutokea eneo hilo na kudai kwamba marehemu  ndiye anayejua sababu ya kupigwa risasi.
“Marehemu baada ya kupigwa risasi ya kwanza alilia kwa uchungu na kupiga kelele kuomba msaada. Hata hivyo, hakuna aliyejitokeza.
“Aliongezwa risasi ya pili sauti yake haikutokea tena, wale watu walitimka na pikipiki ndipo wananchi tukajitokeza, nahisi ni mapenzi,” alisema mwanamke mmoja anayefanya biashara karibu na eneo la tukio.
Baba mzazi aliyejitambulisha kwa jina la Julius Jacob Lwena anayeishi Tabata Tenge, Dar yeye alikuwa na haya ya kusema:
“Kifo cha Dorryce kimeniuma sana, ila napenda kusema kwamba maisha yake kwa undani siyajui sana kwa sababu nilikuwa mbali naye.
“Mara ya kwanza marehemu alipomaliza elimu ya sekondari alijiunga na Chuo cha Polisi Moshi, alirudishwa kutokana na ujauzito.
“Baada ya kujifungua tulimpeleka Chuo cha Utumishi Singida, bahati mbaya akapata mimba ya mwanaume mwingine, ikabidi arudi nyumbani.
“Baada ya kujifungua tulimpeleka chuo cha uhasibu Singida na mauti yamempata alipokuja likizo,” alisema mzee huyo.
Marehemu alizikwa Machi 4, mwaka huu katika Makaburi ya Tabata Segerea jijini Dar. Mungu ailaze pema peponi roho yake. Amina.

MAHEKALU YA MAASKOFU KUFURU


Stori: Jelard Lucas na Makongoro Oging’
MTU akifanya jambo la kupita kawaida lakini zuri watu husema ‘amekufuru’, yaani amefanya kitu kizuri! Imezoeleka hivyo. Sasa kauli hiyo imekuja baada ya Uwazi kufanya uchunguzi wa kina na kuyabaini mahekalu ya maaskofu wa Bongo kwamba nayo ni kufuru!
Ghorofa analomiliki Mwingira.
Katika uchunguzi huo, Uwazi lilitumia muda wa wiki mbili na kubaini kwamba, watumishi hao wa Mungu wapo vizuri na lile neno wanalolihubiri kwamba, kwa Mungu kuna raha, kwa Mungu kuna maisha mazuri na mtu akiyataka ampokee Bwana!
Nabii Mwingira.
UCHUNGUZI ULIPOANZIA
Uchunguzi ulianzia kwa askofu mkuu au Nabii George David ‘Geordavie’ wa Kanisa la Ngurumo ya Upako (N.Y.U) lenye maskani yake jijini Arusha ambapo yeye anadaiwa kuwa na jumba kubwa analoishi na familia yake ndani ya jiji hilo na eneo hilo kupewa jina la ‘Mji wa Daudi’. Huyu amewafunika wenzake kwa ubora wa mjengo na pia utajiri alionao.
Ghorofa la Gwajima.
Habari zinasema mjengo wake huo una mandhari ya kiikulu ukilinganisha na mahekalu ya watumishi wenzake ambao wametajwa kumiliki pia.
Kwa mujibu wa chanzo, mjengo wa nabii huyo aliyejizolea umaarufu kwa kuwa na mfumo wa kiutawala kama ule wa wanasiasa, unapatikana katika Kitongoji cha Njiro, Arusha.
Mchungaji Gwajima.
“Sijawahi kuona askofu au nabii anamiliki jumba la kifahari kama lile, lile ghorofa la ofisi tu pia ni balaa. Tena basi ameweka ulinzi mkubwa sijawahi kuona. Nilibahatika kupata picha ya sebuleni kwake utadhani ikulu. Pia niliwahi kuiona ofisi yake jamani! Jamani! (chanzo kinashangaa).
OFISI ZAKE ANAZIITA STATE HOUSE
 Chanzo kiliendelea kudai kuwa, ofisi za nabii huyo ni maarufu kwa jina la ‘state house’ (ikulu) ambapo pia hapo analindwa kama enzi za akina Mfalme Daudi ndiyo maana hata sehemu anayoishi panaitwa Mji wa Daudi.
MBALI NA HEKALU
Kwa Nabii Geordavie, mbali na kumiliki utajiri ambao umewahi kuandikwa na gazeti hili siku za nyuma, lakini imebainika kwamba ana kituo cha redio kinachojulikana kwa jina Ngurumo ya Upako FM chenye makao yake jijini Arusha.
MAHEKALU YA WENZAKE
Nyumba za maaskofu wengine ambao walizukiwa na Uwazi ni ile ya Mchungaji Kiongozi Josephat Gwajima wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Nabii Josephat Mwingira wa Kanisa la Efatha Ministry, Askofu Zakary Kakobe wa Kanisa la Zakary Kakobe International Ministry (zamani Full Gospel Bible Fellowship ‘F.G.B.F’).
Maaskofu wengine ni Lusekelo Anthony ‘Mzee wa Upako’ wa Kanisa la Maombezi (G.R.C) Ubungo -Kibangu, Mchungaji Kiongozi Getrude Rwakatare wa Kanisa la Assemblies of God Mikocheni ‘B’ na Mchungaji Christopher Mtikila wa Kanisa la Salvation Church, wanatajwa kumiliki mahekalu mazuri nchini.
MCHUNGAJI GWAJIMA  
Mchungaji Gwajima hakamatiki kama Geordavie, kwani anatajwa kuwa na mjengo wenye ghorofa nne maeneo ya Salasala jijini Dar. Gwajima maarufu kwa kurudisha misukule, pia anamiliki magari ya kifahari achilia mbali mabasi yanayotumika kubeba waumini wake kwenda kanisani Kawe jijini Dar.
NABII MWINGIRA
Licha ya kuandamwa na skendo, Nabii Mwingira anamiliki jumba la ghorofa moja Mikocheni B, jijini Dar. Ina ulinzi balaa. Eneo kubwa la jumba hilo ni matumizi ya familia yake.
Pia Mwingira anamiliki Benki ya Efatha iliyopo Mwenge jijini Dar. Anatajwa kuwa miongoni mwa watumishi wa Mungu mabilionea sanjari na baadhi ya viwanja na mashamba anayomiliki.
MAMA RWAKATARE
Mama Rwakatare, wengi humwita ‘Mbaya’. Ni miongoni mwa watumishi wa Mungu waliofanikiwa kujenga nyumba mbili za kisasa, moja ipo Mikocheni B ikiwa na ghorofa moja na Mbezi, Dar yenye ghorofa moja.
MCHUNGAJI MTIKILA
Mchungaji wa Kanisa la Salvation Church, Christopher Mtikila yeye anatajwa kumiliki hekalu moja maeneo ya Mikocheni B jijini Dar likiwa na ghorofa mbili.
MZEE WA UPAKO
Mzee wa Upako ni Mchungaji wa Kanisa la GRC, ni kama Mwingira tu, yeye anamiliki mjengo wa ghorofa moja uliopo Ubungo Kibangu jirani kabisa na kanisa lake.
Mchungaji huyo anatajwa kuwa miongoni mwa watumishi wa Mungu walio vizuri kimaisha. Mzee wa Upako aliwahi kula kiapo katika moja ya vyombo vya habari (jina kapuni) kuwa kwenye maisha yake haamini katika umaskini kwani umaskini siyo sifa nzuri.
ASKOFU KAKOBE
Askofu Kakobe (I.M) anatajwa kumiliki nyumba ya kawaida sana pale Mpakani B, Kijitonyama Dar. Nyumba yake haina ghorofa. Aliwahi kuburuzana mahakamani na baadhi ya waumini kwa madai ya hati miliki ya kanisa.
Jumamosi iliyopita waandishi wetu walifika nyumbani kwake na kubahatika kuzungumza na majirani ambao wengi walikuwa na swali moja ni kwa nini Kakobe hateremshi hekalu la kisasa ilihali fedha anayo?
KUWAPATA ISHU
Miongoni mwa watu wagumu kupatikana na kuzungumza na wanahabari ni watumishi hao wa Mungu ambapo wote walipotafutwa kwa njia zote, simu na kufuatwa makanisani mwao hawakupatikana.
Kuna wakati Mchungaji Lusekelo aliwahi kuulizwa ni kwa nini hawapatikani, alisema hata Yesu alikuwa hapatikani kirahisi!!

MARANDO: BABU SEYA ALIBAMBIKIWA KESI

Na Elvan Stambuli
WAKILI maarufu nchini, Mabere Nyaucho Marando amesema mwanamuziki Nguza Viking ‘Babu Seya’ na watoto wake watatu walimbambikiwa kesi.

Mabere Nyaucho Marando akiongea na waandishi wa Global Publishers (hawapo pichani).
Akizungumza na waandishi wa habari wa Global Publishers katika ofisi zao zilizopo Mwenge Bamaga mwishoni mwa wiki iliyopita, Marando alisema alipitia jalada la kesi hiyo lenye kurasa 1,362 na kugundua kuwa hakuna hata sehemu moja inayomhusisha kigogo mmoja wa nchi, lakini kesi walikuwa wamebambikiwa.
Hakutaja waliombambikia. Baadhi ya mahojiano ya Marando na waandishi wetu yalikuwa kama ifuatavyo:
Mwandishi: Wewe uliwatetea Babu Seya na watoto wake, unaweza kutueleza ilikuwaje ukatafutwa wewe kuwatetea?
Nguza Vicking ‘Babu Seya’ na mwanaye Johnson Nguza ‘Papii Kocha’.
Marando: Kuna rafiki yangu alikuja kuniomba nifanye kazi ile, nilikataa hasa kwa kuwa nami nina watoto wa kike. Baadaye nilikubali kwanza kusoma jalada la kesi lenye kurasa 1,362 nikaona hawakufanya makosa waliyoshitakiwa, walibambikiwa nikaamua kuwatetea katika ngazi ya rufaa, niliwatetea bure kabisa.
Mwandishi: Kama hivyo ndivyo, ina maana makosa walibambikiwa?
Marando: Ndiyo, naamini makosa yale walibambikiwa lakini siyo na kigogo yeyote wa serikali katika nchi hii. Lakini Mahakama ya Rufaa haina makosa, Babu Seya na wanawe walikuwa wamehukumiwa na magazeti. Nyinyi waandishi mlimhukumu kwa hii fabricated case (kesi ya kutunga) na sababu zipo.
Mwandishi: Je, kuna njia yoyote iliyobaki ya kumtoa Babu Seya na mwanaye?
Marando: Mimi kama wakili, hapo ndiyo mwisho wangu, nimenyoosha mikono. Nimeshindwa nusu, nimeshinda nusu (Kwa kuwatoa jela Mbangu na mdogo wake Francis Nguza na kubaki jela Nguza na Papii.)
Mwandishi: Umekuwa Chadema na kuna habari kuwa uliondolewa kuwa mwanasheria wa chama akapewa Tundu Lissu,pia kuna habari kuwa umekosana na mwenyekiti wako, Freeman Mbowe, Je,  kuna ukweli wowote juu ya hayo?
Marando: Sijawahi kuwa mwanasheria wa Chadema isipokuwa wanapokuwa na tatizo la kisheria huwa nawapa ushauri wakihitaji. Mheshimiwa Mbowe sijakosana naye isipokuwa katika vikao tunaweza kutofautiana na hivyo ndivyo chama makini kilivyo. Wote hamuwezi kuwa na wazo moja katika hoja, baadaye inapigwa kura, upande unaoshinda na unaoshindwa huwa kitu kimoja. Hakuna ugomvi hapo, mimi ni Makamu  Mwenyekiti Kanda ya Pwani na Mjumbe wa Kamati Kuu.
Mwandishi: Lipo suala kuwa wewe ni usalama wa taifa na ulihusika na mauaji ya Komandoo Tamim, Je, hilo unaweza kulifafanua?
Marando: Mimi nilijiunga na usalama wa taifa na nilikuwa kitengo cha mambo ya nje hasa kuhusu vyama vya ukombozi enzi hizo. Niliacha kazi hiyo kwa kukabidhi barua kwa aliyekuwa mkurugenzi wake, Dk. Hansy Kitime baada ya kulazimishwa kujiunga na TANU kwani sikuwa mwanachama. Kuhusu Tamim aliuawa mwaka 1983 wakati huo mimi nilikuwa nimeshaacha kazi.
Hili la kuua walikuwa wakinipakazia watu wa usalama wa taifa bila shaka kwa sababu niliacha kazi kijeuri nikawa jobless (sina kazi).
Baadaye nikaajiriwa Shirika la Sheria Tanzania kabla ya kuanzisha kampuni yangu ya uwakili mwaka 1984. Nimefafanua hili mara nyingi sana, nadhani leo mmenielewa na Watanzania watanielewa.

March 07, 2014

Ngumi mkononi bungeni


Mjumbe wa Bunge Maalumu la Katiba, Magdalena Sakaya (kushoto), akizozana na Magdalena Likwina baada ya Semina ya Kupitia Vifungu vya Rasimu ya Kanuni kuahirishwa kutokana na vurugu zilizotokea bungeni jana. Picha na Silvan Kiwale  

Dodoma.
 Ngumi mkononi ndilo neno jepesi ambalo linafaa kutumika baada ya vurugu kubwa kutokea jana ndani ya Ukumbi wa Bunge Maalumu la Katiba kiasi cha kumlazimisha Mwenyekiti wa Muda, Pandu Ameir Kificho kuahirisha semina kabla ya wakati wake.
Semina ya wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba, imekuwa ikianza saa 4:00 asubuhi hadi saa 7:00 mchana kabla ya kuendelea tena kuanzia saa 11:00 jioni hadi saa 3:00 usiku. Jana, katika kipindi cha asubuhi, semina hiyo iliahirishwa saa 6:17 licha ya kuanza saa tano asubuhi kabla ya kurejea tena saa 10 jioni.
Ngumi zilitaka kupigwa baada ya Waziri wa Katiba na Sheria wa Zanzibar, Abubakari Hamis Bakari kuhoji uhalali wa Christopher Ole Sendeka na Ummy Mwalimu kuchangia wakati hawakuwamo katika orodha ya wachangiaji jambo ambalo liliibua mjadala mkali na kurushiana maneno kabla ya Mwenyekiti Pandu Ameir Kificho kuahirisha semina hiyo.
Chanzo cha vurugu
Kificho alimpa Ole Sendeka nafasi ya kuchangia Kifungu namba 58 cha rasimu ya kanuni na baada ya kutoa mchango wake, Hamisi ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati ya Kanuni, alisimama na kumtaka Mwenyekiti Kificho kuacha kuwateua watu ambao hawamo katika orodha ya wachangiaji.
Kificho hakumsikiliza na badala yake, alimpa nafasi mjumbe mwingine wa Bunge hilo Ummy Mwalimu ambaye pia ni Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais, kuchangia. Hata hivyo kabla hajafanya hivyo, Bakari alisimama tena na kumzuia kuchangia kwa madai kuwa hakuwamo kwenye orodha ya wachangiaji.
“Mheshimiwa Mwenyekiti, kama tutaendelea na utaratibu huu suala la kuchangia kanuni linaweza kutupeleka hadi miezi sita bila ya kumaliza. Haya majina hayakuwemo kwenye orodha ya wachangiaji na huyo aliyemaliza sasa Ole Sendeka, naye hakuwamo, naomba tuache mchezo huu,” alisema Bakari.
Aliendelea: “Sekretarieti inakuchomekea majina mwenyekiti na kama hivyo ndivyo, basi tunatakiwa kuwachukulia hatua kali hawa kwani tunataka kujadili hoja ambazo hazimo.”
Bakari alisema wajumbe waliotakiwa kuchangia ni wale ambao walipeleka majina kwa makatibu wa Bunge hilo pamoja na michango yao kwa maandishi ili wapewe nafasi ya kuzungumza, lakini Kificho alikuwa akiwateua wajumbe ambao hawamo katika orodha hiyo.
Kificho ajibu
“Mimi sina tatizo na jambo hilo, mkisema tuendelee basi sawa, lakini mkitaka tufanye mambo kwa uzuri inawezekana pia, jambo la muhimu ni kuwa tupo hapa kutengeneza Katiba ya wananchi siyo ya vyama.”
Kelele zilianza kusikika huku wajumbe wakiimba kuwa mwenyekiti anayumba… na kumtaka mwenyekiti atoke nje na kukiacha kiti, kwani anafanya upendeleo.

Kelele hizo ziliambatana na wajumbe hao kuwasha vipaza sauti bila utaratibu. Mjumbe Sadifa Juma Khamis ndiye aliyekuwa wa kwanza kuwasha kipaza sauti chake na kusimama wakati wote akisema anataka kuchangia, huku akiungwa mkono na wajumbe wengine kadhaa.
Kutokana na tukio hilo, Kificho alilazimika kumwita Mwenyekiti wa Kamati ya Kanuni, Profesa Costa Mahalu ambaye alikiri kuwa yako majina ambayo hayakuwamo kwenye orodha, lakini kwa mwenyekiti yalionekana.
Moto zaidi uliwaka baada ya Ole Sendeka kusimama hata bila ya kupewa nafasi na kusema anazijua kanuni vizuri na kwamba asingeweza kuzivunja.
“Nilijua hayo yote na mimi siyo dhaifu wa kanuni kwani najua kila kitu na tulikwenda tangu mwanzo; mimi, Mheshimiwa Ummy Mwalimu na Peter Serukamba, ndiyo maana majina yetu yamo humo ila kama mapigo yetu yanawakwaza wengine waseme, siyo jukumu la mimi kupeleka mapendekezo yangu kwa Bakari, labda kama wewe una msimamo wako na chama chako,” alisema Ole Sendeka.
Kauli hiyo ilizusha kelele za wajumbe ndani ya ukumbi, huku Kificho akiwatuliza na kusema Ole Sendeka aliteleza ulimi na kumtaka aombe radhi kama anataka, lakini mjumbe huyo aligoma kwa kuonyesha ishara ya mikono, jambo ambalo lilimfanya Bakari kusimama tena.
Bakari alisimama na kueleza uzoefu wake wa miaka 34 kwenye Bunge akijisifu kuwa yeye ni zaidi ya Ole Sendeka.
“Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi sihitaji kuombwa msamaha na Ole Sendeka, nimekuwa kwenye mabunge haya tangu mwaka 1980, leo hii mtu kutoka Simanjiro miaka 10 iliyopita hawezi kunitisha,” alisema Bakari.
Wengine nusura wapigane
Kauli hiyo iliwafanya wajumbe wengi bungeni kusimama, huku wengine wakitaka kupigana ngumi baadhi wakisema: “Twende nje tukapigane, twende nje tukapigane…”
Waliokuwa wakibishana zaidi ni Abdalla Sharia ambaye alitaka kupigana na Khatibu Haji kabla ya kuzuiwa na wenzao, huku Tauhida Nyimbo akitaka kuzikunja na Seleman Bungara (Bwege).
Wakati Bunge likiwa limechafuka na kukiwa na kelele nyingi, mwandishi wa habari hizi alimuona, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, Anne Makinda akimuonyesha kwa ishara ya mikono Kificho kuahirisha semina.
“Naahirisha semina hii mpaka saa kumi jioni,” alisema Kificho na kuwafanya wajumbe kupiga kelele huku wengine wakishangilia na baadhi wakiguna.
Nje ya ukumbi
Wakiwa nje ya ukumbi, Ole Sendeka alisema hoja zake ni nzito na haziwezi kuzimwa na Bakari ambaye anaonekana kuwa na masilahi binafsi.
Alisema yeye pamoja na wenzake (Ummy na Serukamba), bado wanatarajia kuwasha moto kwa kila kifungu ili mambo yaweze kukaa vizuri na kuwa kilichotokea kwake ni burudani.
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alisema tatizo kubwa lililosababisha mambo hayo ni misimamo ya mwenyekiti kuyumba wakati wote.
Hata hivyo, alilaani kitendo cha wajumbe wengine kuwa na hoja alizoziita za kitoto kwa kuzomeazomea akisema hata kama kiti kinayumba, bado walipaswa kuwa watulivu na kuangalia kilichowapeleka Dodoma.
Mjumbe mwingine, Charles Tzeba ambaye pia ni Naibu Waziri wa Uchukuzi, alitetea kauli ya Sendeka na kusema hata kama hakuwa kwenye orodha alipaswa kuchangia kwani hiyo ilikuwa ni semina ambayo kila mtu anayo haki ya kuchangia wakati wowote.
Bunge liliporejea jioni, wajumbe wawili-James Mbatia na Profesa Mark Mwandosya walisimama na kutoa nasaha za kutuliza jazba pale wajumbe wanapokwaruzana, huku Mwenyekiti Kificho akisema kilichotokea asubuhi kilitokana na yeye kutokujua kwamba baadhi ya wajumbe hawakuwa katika orodha.

March 06, 2014

WAUGUZI NA MADAKTARI WASITISHA KUTOA HUDUMA KWA WAGONJWA BAADA YA HOSPITALI KUKUMBWA NA MAFURIKO

 Huu ni mtaro wa kupitisha maji taka ambao umepita katikati ya Hospitali ya Palestina ambapo ulifumuka na kusababisha kusambaa kwa maji machafu katika kila kona ya hospitali hiyo.
 Mmoja wa wagonjwa akiwa anangojea kupata huduma baada ya mvua hiyo kubwa kuisha.
 Haya ni maji machafu ambayo yametapakaa kila sehemu ya hospitali.
 Kushoto ni mgonjwa akiwa amelala juu ya benchi ambapo pembeni kuna maji na matope ambayo yamechanganyikana na kinyesi kutoka katika vyoo mbalimbali katika makazi ya watu.
 Hii ndio hali halisi ya chemba hii ambayo ipo ndani ya Hospitali ya Sinza Palestina.
 Hizi ni chemba zaidi ambazo zipo nje na pia zimeungana na zilizopo ndani ya hospital hiyo.
 Wagonjwa zaidi wakingojea waganga kufika pia kumalizia kusafishwa kwa vyumba hivyo ili wapate kuhudumiwa.
 Moja ya chumba ambacho kilikuwa kimejaa tope kikingojea kusafishwa.
 Hapa hata hapapitiki.
 Baadhi ya viti vikiwa vimeegeshwa kwa ajili ya kufanyiwa usafi.
 Hakuna mtu katika maeneo haya kutokana na mvua kubwa iliyonyesha.
 Kila kitu kimekaa hovyo hovyo baada ya mvua kubwa kunyesha.
 Baadhi ya vifaa vya kutibia wagonjwa vikiwa juu ya moja ya kitanda cha kutibia wagonjwa.
 Huu ndio mtaro wa maji machafu ambapo maji kutoka nje yamepita ndani ya hospitali hiyo na kusababisha maafa baada ya mtaro huo kuziba.
Mapema mchana wa leo kumetokea mvua kubwa katika maeneo mbalimbali ya Jijini Dar es Salaam na kusababisha usumbufu mkubwa baada ya maeneo mengi kukumbwa na tatizo la maji mengi ambayo yaliziba barabara, nyumba za watu pamoja na maeneo mbalimbali.
Mvua hizo kubwa ambazo hata mamlaka ya hali ya hewa wametahadhalisha kwamba zitakuwepo kuanzia Tarehe 5.03.2014 hadi Tarehe 7.03.2014  zimesababisha usumbufu mkubwa katika Hospitali ya Halmashauri ya Kinondoni Sinza - Palestina kujaa maji kila kona na kupelekea wauguzi kuacha kazi na kupanda juu ya meza na viti wakikwepa maji hayo wakati wengine wakikimbia katika eneo hilo kuhofia maji hayo.
Walikwepa maji hayo kutokana na kwamba si ya mvua tu lakini yalikuwa ni machafu yaliyochanganyikana na maji kutoka vyooni ambapo kuna chemba moja ya maji machafu imepita hapo.
Baada ya mvua hiyo kuisha iliwalazimu wafanya usafi wachukue muda wa zaidi ya dakika 30 kufanya usafi na kutoa matope yaliyokuwa yamejaa kila chumba.

Akiongea kwa simu Mganga Mkuu wa Hospitalu hiyo amekili kwamba kuna usumbufu mkubwa wa chemba hiyo na mvua hasa katika kipindi hicho ambapo zinanyesha kwa kiasi kikubwa.
Ameongeza kwa kusema kwamba kunajuhudi zinahitajika kufanyika ili kuweza kunusuru tatizo hilo lisiendelee.

Nao baadhi ya wagonjwa ambao wengine walikuwa katika hali ambayo si nzuri wamesema wanaiomba serikali itazame tatizo hilo maana licha ya maji hayo kuwa mengi lakini pia ni hatari kwa afya zao kwa ujumla.

March 05, 2014

Kardinali Pengo aweka wazi msimamo wa Kanisa

Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Muadhama Polycarp Kardinali Pengo akiwaonesha waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, nakala ya gazeti la Mwanachi lililoandika habari kuhusu msimamo wa Kanisa juu ya suala la serikali tatu.

Dar es Salaam/Iringa.
Siku mbili baada ya Tume ya Haki na Amani ya Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC) kutoa waraka wa kulitaka Bunge Maalumu la Katiba kutopuuza mapendekezo ya muundo wa serikali tatu, Askofu Mkuu wa Jimbo Mkuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo ameibuka na kusema msimamo huo siyo wa Kanisa Katoliki nchini.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Kardinali Pengo pamoja na kukiri kuwa tume ilitoa maoni hayo, alikanusha kuwa taarifa zilizotolewa na moja ya magazeti kuwa msimamo wa Kanisa Katoliki ni serikali tatu.
“Maoni ya Tume hayawezi kuwa ni msimamo wa kanisa. Kanisa Katoliki lina utaratibu wa kutoa misimamo yake na huwa inatolewa na Mwenyekiti wa TEC,” alisema.
Hata hivyo, Rais wa TEC, Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa kutoka Jimbo la Iringa, alisema jana kuwa alikuwa na shughuli nyingi, hivyo asingeweza kuzungumzia suala hilo, labda wiki ijayo.
Akizungumza katika makazi yake mjini Iringa, Askofu Ngalalekumtwa alisema: “Mniache, nina shughuli nyingi…labda mnitafute wiki ijayo,” alisema.
Vilevile, Pengo ambaye alirejea msimamo wake binafsi wa kuunga mkono Muungano wa serikali mbili, alisema kwa namna Rasimu ya Katiba ilivyo, hakuna kigezo cha kulazimisha Kanisa Katoliki litoe msimamo.
Alisema Kanisa Katoliki lingeweza kutoa msimamo iwapo Rasimu ya Katiba ingekuwa na dosari zinazohusu imani au maadili.
“Kwa mfano, (Rasimu) ingekuwa inasema, hakuna Mungu lazima tungekuja juu kwa sababu inaingilia imani yetu,” alisema Kardinali Pengo na kufafanua:
“Vilevile tungeweza kusema inakwenda kinyume na maadili iwapo inaruhusu kuua wazee au inaunga mkono ndoa za jinsi moja.”
Tamko la Tume
Tamko la tume hiyo inayoongozwa na Askofu Mkuu wa Tabora, Paulo Ruzoka liliweka bayana kuwa muundo wa serikali mbili haukutatua matatizo ya msingi na badala yake ulilimbikiza kero zilizosababisha Zanzibar kujiundia katiba yake mwaka 2010 bila kushauriana na Tanzania Bara.
Tamko hilo la kurasa 15 lililosambazwa kwa baadhi ya Wajumbe wa Bunge la Katiba, lilitolewa baada ya mkutano wa kitaifa wa Wajumbe wa Kamati za Majimbo za Haki na Amani za Kanisa hilo na Chama cha Wanataaluma Wakatoliki Tanzania (CPT), uliofanyika jijini Dar es Salaam Februari 5 na 6 mwaka huu.

Msimamo binafsi
Kardinali Pengo alisema katika misimamo ya kisiasa ndani ya Kanisa Katoliki, waumini wanatofautiana bila kuzingatia ni kiongozi au muumini wa kawaida na hakuna sababu ya kulazimishwa kuwa na msimamo unaofanana.
Alisema yeye anaona serikali mbili zinaweza kusaidia zaidi katika usalama wa nchi na kujenga umoja hasa katika kuzuia watu wa nje wenye nia mbaya kupenya nchini ili kuanzisha chokochoko za uvunjifu wa amani.
Alisema ana wasiwasi mfumo wa Serikali tatu utatoa mwanya kwa maadui kupenya Zanzibar na hata kuingia Tanzania Bara.
Alitoa mfano wa nchi jirani ya Kenya, ambako matukio kadhaa makubwa ya kigaidi yametokea na kuonya kuwa kamwe asingependea kuona yanafanyika hapa nchini.
Kura ya siri
Akizungumzia mvutano wa mfumo wa upigani kura kwenye Bunge la Katiba, Pengo alisema: “Kura ya siri ndiyo njia pekee ya kutenda haki katika kupitisha vifungu kwenye Bunge linaloendelea mjini Dodoma.”

Lissu amkubali Sitta


 “Kwanza niseme kuwa mimi Lissu kwa mtazamo wangu binafsi, nakubaliana na uamuzi wa mzee yule (Sitta), hakuna mtu wa kuliweza Bunge hili zaidi yake na kwa vyovyote vile, mambo yatakuwa mazuri mbele yake.” Tundu Lissu  

Dodoma.
Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema) amesema ameupokea kwa furaha, uteuzi na uamuzi wa Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta wa kugombea Uenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba.
Lissu amesema uadilifu na misingi mizuri aliyonayo Sitta itasaidia kupata Katiba ya wananchi badala ya ile ya masilahi ya chama au ya kundi la watu wachache.
Tundu alisema kwa kuzingatia hayo, hakuna sababu ya  watu wengine kutamani kiti hicho kwa sababu  wakiingia katika uchaguzi, wataangushwa na Sitta.
“Kwanza niseme kuwa mimi Lissu kwa mtazamo wangu binafsi, nakubaliana na uamuzi wa mzee yule (Sitta), hakuna mtu wa kuliweza Bunge hili zaidi yake na kwa vyovyote vile, mambo yatakuwa mazuri mbele yake,” alisema Lissu.Alisema katika kipindi ambacho aliongoza Bunge la Tisa, watu wote walimkubali na kuamini kuwa angeweza kuwa kiongozi bora wa Bunge la sasa, lenye changamoto kubwa.
Akizungumzia tetesi kuwa Mwanasheria Mkuu wa zamani,  Andrew Chenge ameonyesha nia  ya kugombea nafasi hiyo, alisema hayuko tayari kumuunga mkono.
Lissu alisema Chenge hataweza  kuliongoza Bunge hilo na kwamba kama atachaguliwa,  litavunjika likiwa mikononi mwake.
Kuhusu Samia Suluhu Hassan anayetajwa kuwania nafasi ya Makamu Mwenyekiti , alisema hana shaka pia ingawa hajaonyesha makeke yake mbele ya vikao muhimu kama vya Bunge, lakini ni mzoefu wa muda mrefu serikalini na katika nafasi mbalimbali.

BUNGE LA KATIBA NGOMA INOGILE!

WAKATI msuguano  wa wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba ukiendelea mjini Dodoma na kuzua majadiliano makali juu ya upigaji kura ya wazi au ya siri, ngoma inogile kwani inatabiriwa kuwa huenda bunge hilo lisifikishe  siku 90 za uhai wake na kuishia siku 70, baadhi wa wajumbe wameliambia Risasi Mchanganyiko.

Wakizungumza bila ya kutaka kutajwa majina yao, baadhi ya wajumbe wa bunge hilo wamesema kuwa hali siyo shwari kutokana na baadhi ya wanasiasa kutetea misimamo yao ili ishinde.
“Tunaonekana si wamoja ndani ya bunge hili na kila upande umekuja na dhamira yake ya kutafuta ushindi, hali hii inaweza kulifanya bunge kushindwa kumaliza siku 90 zilizopangwa kutafuta Katiba Mpya ya Tanzania,” alisema mjumbe mmoja kutoka Zanzibar kwa niaba ya wenzake.
Pia wanasiasa wanaotoka katika vyama vya upinzani wamekuwa wakikishutumu Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kutaka kuuteka mkutano huo.
“Asilimia kubwa ya wapinzani wanataka kura za  siri lakini CCM wanataka wajumbe wapige kura za wazi kwa maslahi yao ili kuweza kuwaadhibu wanachama wao wasiokubaliana na hoja za upande wao, kwa mtazamo huu hatutafika siku 90,” aliongeza mjumbe mwingine wa upinzani.
Kwa upande wao baadhi ya wajumbe  wa CCM wamewashutumu wenzao wa upinzani  kwa kuwaambia kuwa wana malengo  ya  kuvunja muungano wa Tanzania kwa ajili ya uroho wa madaraka.
“Haiwezekani tuje Dodoma kama Watanzania na tutoke  tukiwa si Watanzania, lengo letu ni kudumisha umoja na kuendeleza mazuri ya viongozi wetu waliotangulia,” alisema mbunge wa CCM anayetokea Mwanza.
Naye mwenyekiti wa  muda wa bunge hilo, Pandu Amir Kificho amekuwa katika wakati mgumu kwa kuwataka wajumbe kuacha  kuchangia rasimu ya katiba kabla ya muda wake.
“Naomba nieleweke, bado hatujaingia kuichambua rasimu ya katiba, hebu tujadili kanuni za kutuongoza kwanza,” alikaririwa mwenyekiti huyo akimwambia Profesa Ibrahim Lipumba wa Chama Cha Wananchi (CUF) na kuwafanya wajumbe wengine kumshangilia.
Baadhi ya wadau wanaofuatilia bunge hilo wamesema hawatashangaa kuona wajumbe wakiondoka Dodoma kabla ya kutimia kwa siku 90.
“Hilo liko wazi, fedha za walipa kodi zinaweza kuliwa bure na Watanzania wasipate kile wanachotarajia,” alisema Othman Zinga anayefuatilia mkutano huo.

LAANA YA KANGA MOJA YAINGIA MPAKA KWA WACHEZA SHOW ZA MAJUKWAANI

Toka umeingia huu mtindo wa lile kundi la khanga moko siku hizi kamezuka kamtindo ka wacheza show za jukwaani nao kuvaa khanga na kuonesha sehemu kubwa za maongo yao ikiwemo kufuli walizo vaaa...Hii ni laana ya khanga moko inazidi kutafuna tasnia ya sanaaaaa ....
Umati mkubwa uliofulika katika ukumbi kwenye show moja ya mziki wakishangazwa na Show ya mwanadada huyo hapo juuu baada ya show hiyo kila mtu alisikika akimponda huyo dada kwa kile alichofanya hapo jukwaani

AIBU: KIGOGO ANASWA AKIONGOZANA NA KAHABA ALIYEVALIA NUSU UCHI





Kama kweli uko sawa na una akili timamu huwezi ongozana na mtu amevaa namna hii, kwanza ni aibu kwako kwani inaonyesha na wewe pia umekubaliana na mavazi hayo ya ajabu.